Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Ismail Baqaei, amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea katika mji wa Khuzdar, kusini magharibi mwa Pakistan, ambalo limesababisha vifo na majeruhi wa raia kadhaa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na IRNA, Baqaei alitoa salamu za rambirambi na pole za dhati kwa familia za wahanga, pamoja na serikali na wananchi wa Pakistan, akisisitiza mshikamano wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kipindi hiki cha majonzi.
Msemaji huyo alikumbusha msimamo wa kudumu wa Iran wa kulaani aina zote za ugaidi na misimamo mikali, akieleza kuwa vitendo vya kigaidi haviwezi kuhalalishwa kwa sababu yoyote ile.
Aidha, Baqaei alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano na uratibu kati ya nchi za eneo hili ili kupambana kwa ufanisi na ugaidi, hususan kwa kuwabaini, kuwafuatilia na kuwachukulia hatua wahusika, wapangaji, wafadhili na wote wanaounga mkono vitendo vya kigaidi.
Your Comment